Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Hamis Mwinyimvua amekutana na Kampuni ya Rift Valley Energy inayotaka kuzalisha umeme kwa kutumia nguvu ya upepo Mkoani Njombe.
Dkt.Mwinyimvua
amekutana na Kampuni hiyo katika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati Mkoani
Dodoma.
Katika
mazungumzo hayo Kampuni hiyo imesema kuwa mbali na kutaka kuzalisha Umeme wa
upepo, tayari kampuni hiyo inazalisha umeme wa Megawati 4 kwa kutumia maporomoko
ya maji katika eneo Mwenga mkoani Njombe na kuusambaza kwenye vijiji 34
vinavyozunguka eneo hilo.
Aidha
kampuni hiyo pia itatekeleza miradi mingine ya umeme kwa kutumia maporomoko
madogo ya katika maeneo ya Luponda Mkoani Njombe na Suma Mkoani Mbeya.